[00:20, 9/13/2014] D.J: Mayyah wa shule
Sehemu ya 4
.....unclee, maya aliita. Kwa mshangao mkubwa uncle alitoa macho baada ya kusikia Mayyah akiita jina lake...
Uncleeeee... Mayyah aliendelea kuita, kwa hasira alibamiza mlango na kurudi chumbani kwake akakaa kitandani na kuanza kujilaumu kwa kitendo ambacho alitaka kukifanya na mjomba wake Yaani kaka wa mama yake..lakini swali lingine ambalo lilikuwa linamuwazisha ni kuhusu Pili π mhhhhh Hivi Kweli Pili ana husiano na uncle bila mimi kujua?? kwahiyo uncle alitaka nichanganya mimi na pili?? aliwazaa lakini hakupata jibu, akapanga kumuuliza mjomba wake kuhusu swala hilo
.......................................
Levina ni msichana anayejihusisha na maswala ya urembo shuleni hapo na alikuwa maarufu sana baada ya kushiriki mashindano ya kumtafuta mrembo wa shule....Levina Lucas alikuwa rafiki mkubwa wa Mayyah na siku Hiyo Mayyah aliamua kumueleza Levina kuhusu maswahiba ambayo yalimkuta na mjomba wake,,,,
Mayyah rafiki yangu yule atabaki Kuwa ni mjomba wako tu usithubutu akufanyie kitu chochote kibayaaa. Ile ni laana na aibu, haitaleta picha nzuri....wewe ni msichana mzuri. Muda ukifika tu utapata mtu wako Mayyah........ Mayyah alimshukuru Levina na kuahidi kujitahid kadri ya uwezo wake kuachana na mawazo hayo na kutouliza kabisa kuhusiana na swala la mjomba na Pili
............,..,.......................
Ni mahafali ya kidato cha NNE ambapo Mayyah anamaliza elimu ya secondary na moja kwa moja wazazi wake walimtafutia Chuo cha uandishi wa habari pale DSJ maeneo ya ilala jijini dar............
.............,............................
Mayyah sasa yupo jijini Dar baada ya kukutana na vituko na balaa za kila aina. Anakutana na marafiki wapya na rafiki zake wakuu wakiwa ni bhoke, Irene pamoja na restuta..ambao wote walikuwa wanakaaa hostel moja. Waliishi kwa upendo kama marafiki lakini kila mtu akiwa na tabia zake
.....,.................................
Mayyah alimpoteza baba yake katika ajali mbaya ya gari iliyotokea singida alipokwenda kikazi Mayyah alienda katika mazishi na kurudi. Aliumia sana kumpoteza mzazi wake lakini alimuachia Mungu na kurud kuendelea na masomo
............,.........................
""""""""""Mayyah Hivi nikueleze mara ngapi Kuwa nakupenda?? nitamke neno gani ili ujue nakuhitaji..??
Wewe ni mwanamke mzuri sana na wewe ndo utanifaa maishani. nakupenda sana mayyah
mayyah alikuwa akitafakari maneno ya kijana Patrick aliyowahi kumwambia na mayyah anakumbuka jinsi alivyomjibu """"kuwa hana hadhi ya kuwa na yeye
Mayyah unawaza nini, Irene alimuuliza. Irene nakumbuka jinsi nilivyomjibu Patrick vibaya, natamani hata nimfate nimuombe msamaha.........
Mayyah do you love the guy au kwa Kuwa maisha yamekuwa magumu hapa Chuo na hali ya kifedha sio nzuri ndio umeanza kumuwaza? Nakumbuka ulivyokuwa ukimuelezea vibaya kaka wa watu...Irene alihoji na kuacha kufanya alichokuwa akifanya.. Mayyah alishindwa ajibu lipi kati ya maswali aliyoulizwa
Patrick odwa ni mwanafunzi wa degree pale Chuo cha DSJ. Baba yake ni mganda na mama yake ni mtu wa Mombasa. Alikuwa mrefu, mwenye mwili km mtu aliyetoka gym, alikuwa na rangi nzuri, watu wengi walimfananisha na mcheza mpira wa kikapu. Kilichowavuta wanawake wengi kwake ni macho yake na mashavu ya kubonyea, pia marashi aliyokuwa akipulizia na nguo alizotupia. Kwa kifupi alikuwa kijana ambaye kila mwanamke akimuangalia anamtamani.......Patrick alitokea kumpenda sana Mayyah na akaapa kutumia kila njia kumpata Mayyah ingawaje Mayyah alikuwa akimjibu dry sana.......................
Patrick Patrick Patrick... Mayyah alimuita Patrick ambaye alikuwa anaelekea cafteria. Patrick akageuka na kutabasamu, oooooooh Mayyah mambo................
itaendelea
[00:23, 9/13/2014] D.J: Mayyah wa shule
Sehemu ya 5
Ilipoishia..
Mayyah anamuita Patrick aliyekuwa anaelekea cafteria...
Oohhh mambo Mayyah mzima wewe...mimi mzima patrick....wakabaki wanaangaliana kwa dakika chache
Oooh Mayyah nilikuwa nimekuja kupata chai tunaweza sijui kukaaa wote.ooh woow usijali Patrick let's go..
Mayyah na Patrick walipata break fast na kuongea mambo mengi na kupeana historia za maisha yao walibadilishana namba za simu na kuomba wakutane jumamosi ya siku Hiyo katika sehemu nzuri iliyotulia kwa ajili ya maongezi...
.........................
Ni.jumamosi ya tarehe 22.9.2012 mida ya SAA kumi.jioni Mayyah akiwa na rafiki yake Sara room Mayyah akijaribu Nguo huku Sara akimwambia hii inakufaa au hiii haifai baadae Sara alimchagulia rafiki yake gauni zur la rang ya pink lililoshika mwili wa Mayyah vizur alienda saloon na kuweka nywele katika muonekano mzuri..woow that's my friend Mayyah you look so beautiful..Mayyah alitabasamu..ni mida ya saa kumi na mbili Patrick alikuwa kapaki gari lake nje ya hotel maarufu jijini dar akimsubir Mayyah afike...taratibu alikuwa akinywa wine yake huku akichezea simu....
..................................
Helow Patrick nimeshafika sijui uko kwa wapi...oooh mayaah panda hadi ghorofa ya Pili upande wa kulia utaniona..Patrick hakuamini alipomuona Mayyah akiingia kwa mwndo wa taratibu tabasamu alilolitoa baada ya kumuona Patrick ndilo lililomchanganya patrick......mayah can I hug you? Patrick alishindwa jizuia ikabidi amkumbatie Mayyah na Mayyah. Bila hiana alimpokea na baada ya kuachiana walikaa na Patrick alimtania Mayyah kwa kumwambia your so beautiful...... walikunywa na kula na ndipo hapo ukurasa wa mapenzi ulifunguliwa baina ya Mayyah na patrick..
........... .......................
Ni mida ya sasita Usiku wakiwa kwenye gari Patrick anamwambia Mayyah Kuwa "" kwa sasa ni usiku Mayyah haitakuwa busara wewe kurudi hostel muda huu naona ni vyema kama tukienda kwangu"""" Mayyah hakuwa na ubishi aaaa o ok Patrick kumbe upo out of campus? Yes Mayyah karibu hapa ndo ninaishi..ni self ndogo iliyojitosheleza kwa kila kitu ndani Patrick ni mtoto wa tajiri na bado anasimamia miradi michache ya baba yake......na huyu ni Sossy twizz moja ya marafiki zangu wakubwa nakaa nae hapa....Mayyah alimpa mkono Sossy twiz na kumwambia OK Shem Nashukuru kukufahamu........ni SAA saba Usiku Mayyah akiwa chumbani kwa Patrick wanaamua kuoga na kuingia kitandani..
..................
Patrick anapenda sana movie so anaamua kuweka movie ili waangalie......Mayyah alikuwa akihis hali ya utofaut alitamani sana Patrick auguse mwili wake lakini Patrick walaaa alimkiss tu na kumwambia tulale Mayyah ili kesho uamke jioni nitakupeleka hostel..................
Mahusiano yaayyah na Patrick yalikuwa kwa kasi sana kiasi kwamba yalivuma kwa baadhi ya wanafunz wengine kwani Mayyah alipendeza sio kawaida.........lakini pamoja na hayo yote Mayyah alikuwa akiteseka sana moyoni na kuumia mwanaume anayempenda alikuwa anashindwa kumthini na kujali kama yeye ni mwanamke siku moja aliamua amuite patrick na waongee nae.....
Patrick mpenz wangu najua unanipenda na mimi nakupenda kwa nini lakini unanifanyia Hivi Patrick mimi ni mwanamke tambua kwanini unanitesa kihisiaa....
Sikia Mayyah mpenz nikwambie mimi nakupenda wewe na sijakupendea mapenzi najua una hamu ya kuujua mwili wangu na mimi niujue wako but usijali mpenz muda upo tu tunakaribia mitihani kwa sasa lakini mapenz tutaenjoy tu na tutafanya mpenz ..
Mayyah anampenda sana Patrick ilibidi amuelewe ila siku moja jioni aliamua kumuita restuta na Irene na kuomba waongee kidogo
....................................
Guys nyie ni marafiki zangu na ni kama ndugu zangu naombeni mnisaidie jambo hili kama mnavyojua mimi na Patrick ni wapenz na sasa inaenda miez saba hajawahi nigusa mwili wangu hata siku moja.
irene .ndiye aliyeshangaa sana na kumwambia Kuwa Hapana Mayyah au ana matatizo......haiwezekan Mayyah au unatudanganya Yaani kipind chote cha mapenz yenu Patrick hajawah kukugusa.
Restuta alimtia Mayyah moyo na kumwambia afanye Juu chini wakapime ukimwi labda Patrick mgonjwa na anakupenda so hataki kukuharibia maisha yako....Mayyah alikubaliana na wazo la restuta na kupanga jioni yake aende kwa patrick
Ni jioni Mayyah anaingia kwa Patrick bila hodi anaenda mpaka chumbani na kumkuta Patrick hayupo ingawaje alivyoongea na Patrick alimjibu Kuwa yupo home........Mayyah akapiga simu ya Patrick ikaita akiwa pale pale chumbani na kuamua kuichukua Hiyo simu na kuangalia.........
Itaendelea.............
posted from Bloggeroid